Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis

Ayah by Ayah

Tags

Download Links

Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis translation for Surah Al-Hadid — Ayah 17

57:17
ٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يُحۡيِ ٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ مَوۡتِهَاۚ قَدۡ بَيَّنَّا لَكُمُ ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ ١٧
Jueni kwamba Mwenyezi mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Anaihuisha ardhi kwa mvua baada ya kufa kwake ikatoa mimea. Basi vilevile Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kuhuisha wafu Siku ya Kiyama, na Ndiye Muweza wa kuzilainisha nyoyo baada ya kususuwaa kwake. Kwa hakika tumewafunulia wazi dalili za uweza wetu, huenda nyinyi mkazielewa na kwa hivyo mkawaidhika.