Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis

Ayah by Ayah

Tags

Download Links

Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis translation for Surah Al-Hashr — Ayah 18

59:18
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلۡتَنظُرۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ لِغَدٖۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ ١٨
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo! Muogopeni Mwenyezi Mungu na jihadharini na mateso Yake kwa kuyafanya Aliyowaamrisha na kuyaacha Aliyowakataza, na kila mtu ayazingatie matendo aliyoyatanguliza kwa Siku ya Kiyama. Na muogopeni Mwenyezi Mungu katika kila mnachokitenda na mnachokiacha, hakika Mwenyezi Mungu , Aliyetakasika, ni Mtambuzi wa mnayoyafanya, hakuna chochote kinachofichamana Kwake miongoni mwa matendo yenu, na Yeye ni Mwenye kuwalipa nyinyi kwa hayo.