Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis

Ayah by Ayah

Tags

Download Links

Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis translation for Surah At-Talaq — Ayah 3

65:3
وَيَرۡزُقۡهُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَحۡتَسِبُۚ وَمَن يَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِ فَهُوَ حَسۡبُهُۥٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ بَٰلِغُ أَمۡرِهِۦۚ قَدۡ جَعَلَ ٱللَّهُ لِكُلِّ شَيۡءٖ قَدۡرٗا ٣
na Atamfanyia nyepesi njia za kupata riziki kwa namna ambayo haikupita akilini mwake wala haikuwa kwenye hesabu zake. Na yoyote atakayemtegemea Mwenyezi Mungu basi Yeye Atamtosheleza yale yanayomkera katika mambo yake yote. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kulifikilia jambo Lake, Hapitwi na kitu chochote wala haelemewi na kitu chochote kinachotakikana na Yeye, hakika Mwenyezi Mungu Amekiwekea kila kitu muda wake wa kukomea na kipimo ambacho kitu hiko hakiwezi kukipita.