Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis

Ayah by Ayah

Tags

Download Links

Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis translation for Surah At-Talaq — Ayah 7

65:7
لِيُنفِقۡ ذُو سَعَةٖ مِّن سَعَتِهِۦۖ وَمَن قُدِرَ عَلَيۡهِ رِزۡقُهُۥ فَلۡيُنفِقۡ مِمَّآ ءَاتَىٰهُ ٱللَّهُۚ لَا يُكَلِّفُ ٱللَّهُ نَفۡسًا إِلَّا مَآ ءَاتَىٰهَاۚ سَيَجۡعَلُ ٱللَّهُ بَعۡدَ عُسۡرٖ يُسۡرٗا ٧
Na atoe matumizi mume kulingana na kile alichokunjuliwa nacho na Mwenyezi Mungu kumpa mkewe aliyeachana naye na amlipie mwanawe, iwapo mume ana ukunjufu wa mapato. Na yule ambaye amebanika kimatumizi naye ni fukara, basi na atoe kulingana na kile alichopewa na Mwenyezi Mungu katika matumizi. Masikini halazimishwi kutoa kama kile anacholazimishwa tajiri. Mwenyezi Mungu Ataleta, baada ya dhiki na shida, ukunjufu wa maisha na kutosheka.