Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis

Ayah by Ayah

Tags

Download Links

Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis translation for Surah Al-Ahqaf — Ayah 21

46:21
۞ وَٱذۡكُرۡ أَخَا عَادٍ إِذۡ أَنذَرَ قَوۡمَهُۥ بِٱلۡأَحۡقَافِ وَقَدۡ خَلَتِ ٱلنُّذُرُ مِنۢ بَيۡنِ يَدَيۡهِ وَمِنۡ خَلۡفِهِۦٓ أَلَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّا ٱللَّهَ إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ ٢١
Na kumbuka, ewe Mtume, Nabii wa Mwenyezi Mungu Hūd, ndugu yao kina 'Ād kinasaba na siyo kidini, alipowaonya watu wake kuwa watashukiwa na adhabu ya Mwenyezi Mungu wakiwa kwenye nyumba zao hapo Aḥqāf (mahali kwenye mchanga mwingi) kusini mwa Arabuni. Na kwa hakika wamepita Mitume wakawaonya watu wao kabla ya Hūd na baada yake wakiwaambia, «Msimshirikishe Mwenyezi Mungu na kitu chochote mnapomuabudu. Mimi nawachelea nyinyi adhabu ya Mwenyezi Mungu katika Siku yenye kituko kikubwa , nayo ni Siku ya Kiyama.»