Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis

Ayah by Ayah

Tags

Download Links

Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr and Sheikh Nasir Khamis translation for Surah Al-Fath — Ayah 1

48:1
إِنَّا فَتَحۡنَا لَكَ فَتۡحٗا مُّبِينٗا ١
Sisi tumekufungulia wewe, ewe Mtume, ufunguzi ulio waziwazi, ambao ndani yake Mwenyezi Mungu Ataipa nguvu Dini Yako na Atakupa ushindi juu ya maadui wako, nao ni mapatano ya Ḥudaybiyah ambayo kwayo watu walikuwa katika hali ya amani, na likapanuka duara la ulinganizi wa Dini ya Mwenyezi Mungu, na watu wakaingia kwenye Dini ya Mwenyezi Mungu mapote kwa mapote. Kwa hivyo, Mwenyezi Mung Aliyaita mapatano hayo “Ufunguzi uliofunuka” yaani uliokuwa wazi wenye kujitokeza.